AFRICAN SPORTS, MOJA YA VINARA WA LIGI DARAJA LA KWANZA... |
Mechi za raundi ya 20, 21
na 22 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote zimesimamishwa ili
kupisha Polisi Mara imalize mechi zake za viporo, na timu zote zicheze mechi
zao za raundi zilizobaki kwa pamoja.
Polisi Mara ilifungiwa
kutumia Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma kutokana na vurugu
zilizojitokeza kwenye mechi zake, hivyo kusababisha kuwepo kwa mechi hizo za
viporo dhidi ya JKT Kanembwa na Polisi Tabora.
Tayari Polisi Mara
tumeiruhusu itumie tena Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kwa mechi zake za
nyumbani baada ya kuipa onyo kali kutokana na vurugu hizo. Lakini pia mechi
zake kwenye uwanja huo zitachezwa chini ya uangalizi.
Uamuzi wa kupisha Polisi
Mara imalize mechi zake za viporo una lengo la kuhakikisha mechi zote za raundi
tatu za mwisho zinachezwa pamoja ili kuepuka uwezekano wa kupanga matokeo.
Pia klabu za FDL zenyewe
ziliwasilisha ombi la kutaka mechi hizo za mwisho zichezwe kwa wakati mmoja.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania
(TPLB) wakati wowote kuanzia kesho (Januari 27 mwaka huu) itatoa ratiba ya
mechi za viporo za Polisi Mara, pamoja na tarehe mpya za mechi za raundi ya 20,
21 na 22.
0 COMMENTS:
Post a Comment