Mabeki wa Ruvu Shooting wamemtaja mshambuliaji
wa Yanga, raia wa Burundi, Amissi Tambwe kuwa ndiye mchezaji tishio katika
kikosi cha timu hiyo kwa kile walichodai kuwa anajua majukumu yake anapopata
nafasi ya kufunga.
Hali hiyo ndiyo hasa iliyowafanya wamchunge
zaidi kuliko mchezaji mwingi wa Yanga katika mechi yao ya juzi Jumamosi ya Ligi
Kuu Bara iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar na kumalizika kwa suluhu.
Beki wa
kati wa Ruvu Shooting, George Michael Osei, alisema kabla ya mechi hiyo, kocha wao
mkuu, Tom Olaba, aliwaambia kuwa mtu wa kuchungwa zaidi katika mechi hiyo ni
Tambwe, hivyo kila mchezaji atumie mbinu yoyote ile kumwondoa mchezoni.
Alisema ndiyo maana baada ya kuanza kwa mechi
hiyo, wachezaji wote wa timu hiyo walitumia mbinu hiyo kwa kuwagongagonga wale
wa Yanga na mwisho wa siku wakafanikiwa kuwaondoa mchezoni.
“Tusingefanya hivyo hakika Tambwe lazima
angetufunga, kwani ni mshambuliaji mjanja sana anapokuwa ndani ya eneo la
hatari, hivyo bila ya kuwa makini angetuumiza.
“Washambuliaji wengine wa Yanga ni wa kawaida
sana na hawana utulivu wanapopata nafasi za kufunga, ndiyo maana walikosa nafasi
nyingi za kufunga tofauti na Tambwe ambaye alipata mbili, moja alifunga kwa
mkono na mwamuzi akalikataa bao hilo lakini pia alipiga shuti kali ambalo
lilituogopesha wote,” alisema Osei.
Watu wanajisifia ujinga walioufanya uwanjani,na picha zinaonyesha
ReplyDeletelakini cha kushangaza TFF wanalifumbia macho.