Kocha Mkuu wa Mwadui, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’
amefunguka kuwa kwa sasa kiwango chake cha ukocha siyo cha kuwa msaidizi tena
hapa nchini na kama kuna timu itamhitaji lazima ikubali awe kocha mkuu.
Kauli hiyo inakuja kukiwa na tetesi kuwa Kocha
Msaidizi wa Simba, Selemani Matola yupo mbioni kuondoka klabuni hapo na hivyo,
msaidizi wa Goran Kopunovic anahitajika.
Julio ambaye ni mchezaji na kocha wa zamani wa
Simba, amesema kuwa kama atahitajika klabuni hapo, uwezo wake ni kuwa kocha
mkuu nafasi inayoshikiliwa na Kopunovic na siyo kuwa msaidizi kwa mara
nyingine.
“Kwa sasa nina sifa zote za kuwa kocha mkuu na
siyo kocha msaidizi, ndiyo maana nipo na timu yangu hii, hata kama ipo daraja
la kwanza nina uwezo wa kuwa kocha mkuu Simba, Azam, JKT Ruvu na popote pale
lakini siyo usaidizi tena,” alisema Julio ambaye alidai ana Leseni A ya ukocha
ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf).
“Naamini naweza kufundisha mahali popote na
sichagui iwe ligi kuu au daraja la kwanza kwa sababu ni profesheno yangu na
ndiyo maana nimejiendeleza na kuweza kufika hapa na kuwa mwalimu bora,”
aliongeza Julio.







0 COMMENTS:
Post a Comment