Wachezaji watano wa Mtibwa
Sugar, tena wale muhimu, mikataba yao imefikia tamati na wamegoma kuongeza
mipya!
Nyota wanaotajwa kutangaza nia
ya kuondoka ni kipa tegemeo Said Mohammed, Salim Mbonde na Henry Joseph
Shindika, ambaye alisaini miezi sita katikati ya msimu huu baada ya kuachana na
Simba mwishoni mwa msimu uliopita.
Habari za kina zinasema
kuwa, Mohammed yupo mguu ndani-nje kujiunga na mabingwa watetezi, Azam, Mbonde
anawindwa na Simba huku Shindika yeye akifunguka mwenyewe kuwa kwa sasa hawezi
kuongeza mkataba mwingine hadi msimu umalizike huku akikaribisha timu yoyote.
“Mkataba wangu unaisha na
bado sijafanya mazungumzo na mtu yeyote mpaka sasa, hata hivyo sipo tayari kwa
kipindi hiki. Nasikilizia kwanza upepo wa dili kwenye usajili, unajua unaweza
kupata dili la maana kwenye kipindi cha usajili. Iwapo kutakuwa na timu
inanitaka, basi niko tayari kuisikiliza hata sasa hivi,” alisema nyota huyo wa
zamani wa Simba na Taifa Stars.
Msemaji wa Mtibwa, Thobias
Kifaru, alikiri kuwepo kwa dalili za nyota wao kutaka kuondoka lakini akasema
watakaa chini kuzungumza nao.
“Kwa sasa timu inaonekana
kupooza kabisa, nafikiri ni kutokana na matokeo mabaya, lakini wajue ni upepo
tu unapita, kesho keshokutwa tutakaa sawa, suala la msingi tutakaa nao
kuangalia jinsi ya kuboresha mikataba yao,” alisem Kifaru.
Timu hiyo imeambualia
pointi moja katika mechi tano za hivi karibuni na kushushwa kutoka kileleni
hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi kuu, ambayo inaongozwa na mabingwa wa
kihistoria, Yanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment