February 4, 2015

 
BARAKA SHELUKINDO (KULIA) AKIWA NA BARBRA...

Kampuni ya Multichoice leo imezindua rasmi king’amuzi chake cha HDZAPA chenye ubora zaidi katika picha zake na ‘applicationi’ ya DStv now  maalumu kwa ajili ya simu, laptop, tablets na hii ni kwa wateja pekee wa ving’amuzi vya Dstv.

King’amuzi hicho chenye ubora na uwezo  wa hali ya juu na mvuta katika picha zake kwa kiwango cha juu cha sauti ‘dolby digital5.1 .
SHELUKINDO...
Akizungumza na  katika uzinduzi huo, Meneja Uendeshaji wa Dstv, Ronald Baraka Shelukindo alisema king’amuzi hicho na huduma hiyo itakuwa ya kipekee kwa watanzania na watapata fursa kuangali chaneli tofauti huku picha zikiwa ubora wa hali ya juu.
FURAHA NA BARBRA

“ Tumezindua king’amuzi chetu kipya  cha Dstv HDZAPA ambayo itakuwa na picha zenye ubora wa hali ya juu kuliko ving’amuzi vya awali  pamoja na huduma ya Dstv Now ambayo itamrahisishia mteja wetu kuweza kuangalia  chaneli na vipindi tofauti tofauti kupitia simu ya mkononi, tablets, laptop kama atakuwa ni mteja halali lakini.

“Na sasa vipo katika  nchini nzima kwa mawakala wetu kwa wateja wapya wa Dstv watanunua kwa shilingi 99000  na wale wazamani ukienda na king’amuzi cha awali utalipia kiasi cha shilingi 39000 tu,”alisema Shelukindo.


 
FURAHA...

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic