March 13, 2015

Kiungo Mbrazil, Andrey Coutinho ameeleza wazi namna goti linalomuuma linavyomchanganya.


Coutinho ni majeruhi na dalili zote zinaonyesha ataikosa mechi dhidi ya Platinum ya Zimbabwe, Jumapili.

Hali hiyo inamfanya azidi kuwa na hofu ya kuendelea kubaki benchi licha ya juhudi kubwa za Yanga kuhakikisha anarejea.

“Bado, lakini naendelea kupata matibabu. Goti linanibakiza nje na mimi sipendi kukaa benchi,” alisema Coutinho.

“Huenda hivi karibuni mambo yakawa mazuri, nitafurahi nikirejea,” aliongeza.


Katika mazoezi ya leo ya Yanga, Coutinho aliendelea kukaa nje akishuhudia wenzake wakikitimua na baadaye alifanya mazoezi mepesi kabisa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic