Kocha wa Mtibwa Sugar, Meck Maxime amesema wana imani ya kufanya vizuri dhidi ya Simba kesho.
Maxime amesema wamejiandaa
vilivyo na kinachotakiwa kwao ni kujiamini na kupambana.
“Unakumbuka tumepita katika
wakati mgumu sana lakini hakuna aliyekata tamaa.
“Kamwe hatujawahi
kuwadharau Simba. Hata mechi ya mzunguko wa kwanza tulisema wamecheza vizuri na
tukatoka sare.
“Tunajua watakuwa nyumbani,
lakini mpira wa sasa haujali ugenini au nyumbani, tutapambana,” alisisitiza.
Simba inashuka dimbani Uwanja wa Taifa, Dar, kesho kuwavaa Mtibwa katika mechi ya Ligi Kuu Bara.








0 COMMENTS:
Post a Comment