Ile ishu ya mshambuliaji
wa Simba, Ibrahim Ajibu la kuitumikia klabu hiyo kwenye mechi za ligi kuu wiki
iliyopita dhidi ya Prisons na Yanga huku akiwa na kadi nne za njano, linatarajiwa
kuchukua sura mpya katika Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
utakaofanyika leo na kesho mkoani Morogoro.
TFF ilimruhusu Ajibu
kuitumikia Simba katika mechi hizo, ikitumia kanuni mpya za ligi hiyo ambazo
zilikuwa bado hazijapata baraka za mkutano mkuu wa shirikisho hilo.
Jambo hilo lilizua utata
mkubwa na kusababisha maneno mengi huku uongozi wa Yanga ukidai kuwa
utahakikisha unachukua hatua kwa kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa TFF.
Baadhi ya wajumbe wa
mkutano huo, wamesema watahakikisha suala hilo linajadiliwa
ili kukomesha vitendo vya baadhi ya viongozi wa TFF kujichukulia uamuzi mkononi
bila ya kufuata taratibu.
“Hakika watendaji wetu
wamekuwa wakichemka vibaya sana, hii inasikitisha na inashangaza sana kwani
siku zote tunatambua kuwa sheria haiwezi kutumika kama haijapata baraka za rais.
“Hivyohivyo pia katika soka
kanuni zetu haziwezi kutumika kama hazijapata baraka za mkutano mkuu, kwa hiyo jambo
hilo itabidi tuhakikishe linajadiliwa ili upuuzi uliopo wa watu kujiamulia mambo
wao wenyewe uweze kukoma kwa faida ya soka letu,” walisema viongozi hao ambao
waliomba kutotajwa majina yao gazetini.








0 COMMENTS:
Post a Comment