March 18, 2015

MAFTAH 'PELE WA MWANZA' (KULIA) AKIWA NA LUNYAMILA WAKATI WA KUUAGA MWILI WA KOCHA MARSH JIJINI MWANZA.
Wanasoka wa zamani wa Simba na Yanga, Juma Amir Maftah 'Pele wa Mwanza' na Edibily Lunyamila wameeleza kuhuzinishwa kwao na msiba wa Kocha Sylvester Marsh.

Marsh alifariki jijini Dar es Salaam, Jumamosi iliyopita na kusafirishwa na kuzikwa jijini Mwanza, jana.

Lunyamila aliyesafiri hadi Mwanza, amesema Marsh alikuwa ni sehemu ya makocha bora wanaochipukia kufikia kuitwa mahiri na tegemeo la soka la vijana, lakini sasa hatukonaye.

“Mungu anachukua uamuzi usiokosolewa. Lakini Marsh alikuwa muhimu kila mtu anajua. Mimi sikupenda namna alivyosaidiwa na hasa na wahusika wakuu kama TFF. Lakini yote tumuachie Mungu.

“Kikubwa ni watu kuiga mfano wake kwa kuwajali zaidi vijana ambao aliwapa kipaumbele kwa kiasi kikubwa,” alisema.
Kwa upande wa Maftah aliyewahi kung’ara akiwa Pamba, Simba na Taifa Stars, alisema Marsh alikuwa tegemeo la maisha ya soka na hasa kwa vijana.

“Alikuwa akiibua vijana, makocha wengi wamefuata mfano wake. Kwetu hapa Mwanza kila mtu anaujua mchango wake.


“Lakini amevuka zaidi hadi kuwa tegemeo la nchini. Vizuri tumuenzi kwa ubora wa kazi zake,” alisema Pele.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic