March 13, 2015

Mmoja wa viungo wenye uwezo wa juu ni Haruna Moshi ‘Boban’. Lakini siku hizi ameadimika na amekuwa akifanya mazoezi binafsi.


Mmoja wa wadau wa soka na kiongozi wa Villa Squad, Iddi Godigodi ametupia picha Boban akijaribu kumdhibiti mshambuliaji ‘hatari’ Nassor Bin Slum.

Katika picha hiyo ya mtandao wa kijamii aliyotupia Godigodi, inaonekana Boban akijaribu kumba Bin Slum akiwa kwenye mwendo.

Fitness ya Bin Slum inaonekana kuwa juu na Boban anayumba akiwa njiani kuelekea kulamba mchanga.

Walioiona picha hiyo, maswali yao” Huyu huyu Bin Slum anayezidhamini Mbeya City, Stand  United na Wana Ndanda kucheeree yuko fiti hivi”.

Wengine: “Boban kwa ameisha kiasi hicho?” basi kila mmoja ana swali lake.

Lakini ukweli katika picha unaonyesha Boban amezidiwa na mshambuliaji huyo ambaye alikuwa majeruhi, sasa amerejea dimbani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic