Juhudi za Tanzania kufanya
vizuri katika soka la ufukweni zimeanza kupotea baada ya kuchapwa kwa mabao 6-2
wakiwa nyumbani jijini Dar es
Salaam.
Misri ambao ni wazoefu wa
michuano hiyo wameichapa Tanzania kwa mabao 6-2 katika mechi ya kwanza kuwania
kucheza Kombe la Mataifa Afrika iliyopigwa kwenye ufukwe wa Escape One jijini
Dar.
Tanzania ndiyo ilianza
kufunga mabao mawili huku ikionekana kama watoto hao wa Falao wamepotea.
Lakini walianza kurejesha
bao moja baada ya jingine hadi yalipofikia sita.
Uzoefu mkubwa walionao
katika mchezo huo ulionekana ni mzigo kwa vijana wa Tanzania ambao walionyesha
juhudi ambazo hata hivyo hazikuzaa matunda.
Tanzania imekutana na Misri
baada ya kuitoa Kenya kwa kuichapa nyumbani Dar na ugenini Mombasa.







0 COMMENTS:
Post a Comment