March 12, 2015



Suala la muonekano mpya wa kipa wa Simba, Ivo Mapunda akiwa na ndevu zenye rangi limezua gumzo nchini Kenya.


Baadhi ya mitandao ya kijamii hasa kwenye Twitter na Facebook, mashabiki wa soka nchini Kenya wamekuwa wakijadili ubora wa kipa huyo wa zamani wa Gor Mahia ambako alipata umaarufu mkubwa.

Mashabiki hao wamesema Ivo yuko katika kiwango bora kabisa, lakini wengine wamekuwa wakisisitiza kwamba kipa huyo aliwatisha washambuliaji Yanga kwa kutumia ndevu zake wakati timu hiyo iliposhinda kwa bao 1-0.

Ivo aling’ara akiwa katika lango siku hiyo, ilikuwa pia ni siku ya kwanza kuonekana akiwa na ndevu zenye rangi.

Aliokoa hatari kadhaa, yakiwemo mashuti mawili ya Mrisho Ngassa na Hussein Javu huku wengi wakiamini mipira hiyo ilikuwa inatinga wavuni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic