April 13, 2015


Straika wa Yanga, raia wa Burundi, Amissi Tambwe, ameweka bonge la rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick (mabao matatu mechi moja) tatu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mrundi huyo, ni mchezaji pekee aliyeweka rekodi hiyo ambayo haijawahi kuwekwa na mchezaji yeyote tangu uwanja huo ulipoanza kutumika.

Tambwe, mechi yake ya kwanza kufunga hat trick kwenye uwanja huo ilikuwa ni Februari Mosi, 2014 dhidi ya JKT Oljoro akiwa na Simba ambayo ilishinda 4-0.

Mechi nyingine ambayo Mrundi huyo alifunga hat trick ilikuwa ni Septemba 19, 2014 dhidi ya Mgambo JKT ambayo timu yake ya Simba ilipata ushindi mnono wa mabao 6-0.

Mshambuliaji huyo alikamilisha rekodi yake ya kupiga hat-trick ya tatu wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa kwa kufunga mabao manne katika ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya Coastal Union iliyocheza na Yanga.

Tambwe aliyekuwa mfungaji bora msimu uliopita wa ligi kuu akifunga mabao 19, alitua kuichezea Yanga kwenye usajili wa dirisha dogo msimu huu akitokea Simba baada ya kumsitishia mkataba wake kabla ya kutua Jangwani.

Upo uwezekano mkubwa wa mshambuliaji huyo kukitetea kiatu chake cha dhahabu kutokana na kasi yake kubwa aliyonayo hivi sasa ya kufunga mabao.

Mrundi huyo, hadi hivi sasa amefanikiwa kufunga mabao 9, akiongozwa na Simon Msuva mwenye 13 akifuatiwa na mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu aliyepachika 10 na Rashid Mandawa wa Kagera Sugar ambaye naye ana mabao 10.


Kati ya hat-trick hizo alizozipiga, idadi kubwa ya mabao amefunga kwa kichwa kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufunga aina hiyo ya mabao huku mengine kwa kumchambua kipa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic