Basi lililobeba mashabiki wa Yanga wanaokwenda
kuishangilia timu yao keshokutwa, tayari limewasili nchini Zimbabwe.
Basi hilo aina ya Toyota Costa ‘Mayai’ limetua
kwenye mpaka wa Zimbabwe leo asubuhi na walitarajia kukanyaga ardhi ya nchi
hiyo leo.
Hata hivyo, bado watakuwa na safari ndefu na
wanatarajiwa kuwasili Harare leo mchana kabla ya kuanza safari nyingine ya
kwenda Bulawayo ambako Yanga itapambana na FC Platinum katika mchezo wa pili wa
Kombe la Shirikisho.
Mmoja wa mashabiki walio katika basi hilo
amesema wamekuwa wakiendelea vizuri. Msafara wa basi hilo, pia yumo mzee wa
Yanga, Ibrahim Akilimali ambaye ameungana na vijana kwenda kuwapa nguvu Yanga.
Yanga itashuka dimbani Jumamosi kuhakikisha
inalinda ushindi wake wa mabao 5-1 ilioupata jijini Dar ili isonge mbele.
Tunaomba Mungu wetu awape ulinzi.
ReplyDelete