Mbrazil Coutinho amesema kikosi cha Yanga sasa kiko katika kiwango cha juu hali inayozidi kumtia wazimu.
Coutinho ambaye amekaa nje kwa wiki kadhaa kutokana na kuwa majeruhi, amesema anatamani kucheza na kuisaidia timu yake.
"Nimeanza mazoezi taratibu, lakini naona kama nachelewa maana kikosi kinazidi kuimarika na kutamanisha kucheza.
"Natamani niwasaidie wenzangu lakini najivunia namna wanavyoonyesha kiwango cha juu," alisema.
Coutinho alikuwa jukwaani kwenye Uwanja wa Taifa, Dar wakati Yanga ikiitungua Coastal Union kwa mabao 8-0, jana.
Jangwani imenoga bwana,hilo halina ubishi.
ReplyDelete