May 11, 2015

 
ABDI KASSIM AKIPAMBANA DHIDI YA EL HADJI DIOUF KATIKA YA MECHI WAKATI TIMU ZAO ZILIPOKUTANA.
Kiungo wa zamani wa Yanga, Abdi Kassim ‘Babi’ sasa amekuwa lulu nchini Malaysia ambako anaichezea timu ya Ligi Kuu Malaysia, University Technology Mara FC (UiTM).

Babi ambaye timu yake sasa iko katika nafasi ya sita, tayari amezivutia kutoka nchini Bahrain na Korea Kusini.

Mtanzania huyo ambaye ni tegemeo katika kiungo cha UiTM amezivutia timu hizo na tayari zimewasiliana na klabu yake kutaka kujua zaidi kuhusiana naye.

“Kweli wametuma maombi ya kutaka watumie video zangu zaidi, pia profile kuhusiana na nilikocheza kabla ya kuja hapa,” alisema Babi alipozungumza na SALEHJEMBE.


“Baada ya hapo, sijajua nini kitakachofuata lakini mimi nimekuwa nikiendelea kupambana vilivyo kuhakikisha timu yangu inafanya vizuri,” alisisitiza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic