May 30, 2015


Kiungo mkabaji wa zamani wa Simba na Yanga, Athumani Idd ‘Chuji’, amepanga kufunga safari kwenda mkoani Shinyanga kwa ajili ya kusaini mkataba mpya wa kuichezea timu hiyo msimu ujao kwenye Ligi Kuu Bara.

Mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji wakongwe walioiwezesha timu hiyo kupanda kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao, wengine ni Monja Liseki, Juma Jabu, Abdallah Kigodeko na Uhuru Selemani.

Chuji amesema: “Juni 9 nitaenda kusaini mkataba Mwadui kwani uongozi umeniambia nifanye hivyo mimi na wenzangu wote ambao tupo Dar es Salaam.

Hata hivyo Chuji alisisitiza kabla ya kusaini, watajadiliana suala la maslahi kama ilivyo kawaida, kama watakubaliana abasi atafanya hivyo.

“Hatutasaini kichwakichwa kwani tutazungumza kwanza kuhusu maslahi.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic