May 30, 2015


Winga Ramadhan Singano ‘Messi’ anapingana na Simba kuhusu uhalali wa muda wa mkataba wake na kuna uwezekano ukawa mwisho wa mkataba wake kuitumikia timu hiyo.


Hata hivyo, anaweza kujifariji kwani Azam FC imesema inafuatilia kwa kila hatua malumbano hayo na yakiisha tu itamsajili Messi ili kuongeza nguvu katika safu yake ya ushambuliaji.

Kwa siku tatu sasa, Messi amekuwa akisisitiza anamaliza mkataba wake wa miaka miwili kuitumikia Simba aliosaini mwaka juzi, lakini Simba inasisitiza bado mwaka mmoja katika mkataba wake kwani alisaini miaka mitatu.

Messi akasisitiza kuwa kuna wajanja waliobadili vipengele vya mkataba wake uliopelekwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ndipo Azam ilipojitanua na kusema; “Messi maliza matatizo yako uje usaini mkataba huku.”

Katibu Mkuu wa Azam, Idrisa Nassor alisema: “Tunamtaka Messi amalize matatizo yake na Simba halafu aje tuzungumze naye halafu tukikubaliana tumsajili.”

Nassor alisema Messi ni aina ya wachezaji wanaowahitaji kwa ajili ya kuwasajili katika kukiimarisha kikosi chao katika kuelekea michuano ya kimataifa itakayoshiriki ambayo ni Kombe la Shirikisho na Kombe la Kagame.

“Wakati tukionyesha nia ya kumsajili, tumetoa masharti yafuatayo, kwanza kabisa kumaliza matatizo ya kimkataba kati yake na uongozi wa Simba.


“Kama akimalizana nao, basi sisi tutakaa naye meza moja kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kumsainisha mkataba wa kuichezea Azam,” alisema Nassoro huku habari za ndani zikieleza kuwa timu hiyo imeachana na kiungo Amri Kiemba aliyekuwa akiichezea kwa mkopo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic