AKISAINI MBELE YA MANARA... |
Mshambuliaji Mzimbabwe, Justice
Majabvi amesajili mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba na kusema,
anajiamini.
Majabvi amesema anaamini
usajili wake Simba utakuwa na matunda kwa kuwa anaamini uwezo wake pia kikosi
cha Simba.
“Simba ni timu bora
kabisa, nimekaa siku chache hapa lakini nimeona kuna mengi ya kujifunza, pia ni
kikosi chenye ushindani mkubwa kwa kuwa kimejaza wachezaji wenye vipaji.
“Ninaamini tutashirikiana
vizuri na kuisaidia Simba, najiamini. Pia ninawaamini wenzangu,” alisema.
Mzimbabwe huyo alisaini
mkataba wake huo mbele ya msemaji wa Simba, Haji Manara.
0 COMMENTS:
Post a Comment