NAFTALI (KUSHOTO) AKIMKABA OLUNGA ANAYEJARIBU MBINU KUMTOKA... |
Unamkumbuka yule beki wa zamani wa Simba, David
Naftali.
Jamaa fulani mkimya hivi na amepotea muda
mrefu, lakini amefanikiwa kupasua na sasa anakipiga nchini Kenya.
Juzi ameonyesha uwezo mkubwa akiichezea timu ya
mapato ya Kenya (KRA) kwa kumthibiti vilivyo mshambuliaji Michael Olunga wa Gor
Mahia.
Naftali alimkamata Olunga vilivyo ingawa KRA
ilifungwa kwa mabao 2-0, lakini Olunga hakufunga hata moja.
Hali hiyo ilimfanya Olunga kuwa na jazba, kwani
hata mipira ya kichwa ilikuwa ni kazi kupiga kwa kuwa Naftali naye ni ‘mtu
kweli’.
0 COMMENTS:
Post a Comment