MAVUGO, AMESHINDWA KUJIUNGA NA SIMBA... |
Mshambuliaji Kelvin Ndayisenga raia wa Burundi
ametua nchini leo saa 1 usiku tayari kufanya majaribio
katika kikosi cha Simba.
Simba imeendelea na harakati zake za kusaka mshambuliaji ikiwa ni siku chache baada ya kupata uhakika mshambuliaji Laudit Mavugo hatakuja nchini kujiunga na nayo.
Mrundi huyo anayetokea katika kikosi cha AO Bujumbura ametua nchini na kujichimbia
katika moja ya hoteli bora nchini ya Sapphire Garden Court.
Kwa mujibu wa uongozi wa Simba, Ndayisenga
atakabidhiwa kwa Kocha Dylan Kerr raia wa Uingereza ambaye atakuwa na kazi ya
kumhakiki mshambuliaji huyo.
“Kweli amewasili leo na jukumu atakabidhiwa kocha
Kerr na benchi lake la ufundi kuamua kuwa wanamuonaje.
“Kwa sasa dirisha la usajili limesogezwa mbele, hivyo kinachofuata sasa ni suala la la kumalizia usajili,” kilieleza chanzo.
0 COMMENTS:
Post a Comment