August 7, 2015

MWENYEKITI WA KAMATI YA USAJILI YA SIMBA, ZACHARIA HANS POPPE

Unaweza ukasema hii sasa sifa, maana Simba ndani ya siku tatu itakuwa imeshusha wachezaji watatu wa kimataifa kwa ajili ya majaribio.


Kwanza leo imeanza na Mshambuliaji Kelvin Ndayisenga raia wa Burundi ambaye ametokea AO Bujumbura ya kwao Burundi na anatarajia kuanza majaribio mara moja.

Lakini kesho alfajiri, kipa Ricardo Andrade anatua nchi tayari kuanza majaribio. Kipa huyo raia wa Brazil alikuwa anakipiga katika klabu ya Sporting ya nchini Ureno.

Wakati kipa huyo atakuwa amekamilisha idadi ya wachezaji wawili wapya wa kigeni waliotua nchini ndani ya siku mbili, raia wa Mali, atatua Jumatatu.

Huyo ni  Makani Dembele kutoka kutoka katika kikosi kikongwe cha JS Kabylie cha Algeria.

Rais wa Simba, Evans Aveva ameiambia SALEHJEMBE, kwamba ni katika harakati zao za kuhakikisha wanajenga kikosi chao.
“Yote ni mikakati ya usajili, kamati ya usajili kwa kushirikiana na benchi la ufundi pamoja na kamati ya utendaji, imekuwa ikiendelea na kazi zake,” alisema Aveva.


Kesho ni siku muhimu kwa Simba, maarufu kama Simba Day na mashabiki wa Simba watapata nafasi ya kuwaona wachezaji hao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic