Yanga imeitwanga Mbeya City kwa
kuichapa kwa mabao 3-2 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa leo kwenye Uwanja wa
Sokoine mjini Mbeya.
Yanga ambayo imepiga kambi Tukuyu ilionyesha
soka safi na kuibana Mbeya City iliyokuwa nyumbani.
Mabao ya Yanga yalitupiwa kambani na
wageni tu, alianza Andre Coutinho raia wa Brazil.
Baada ya hapo, Amissi Tambwe akatupia
la pili kabla ya Donald Ngoma raia wa Zimbabwe kupiga la tatu.
Mabao ya Mbeya City yamefungwa na Bakari Slang na Joseph Mahundi aliyefunga katika dakika ya 90.
0 COMMENTS:
Post a Comment