Wakati Kocha Louis van Gaal ameamua kuanza Ligi Kuu
England kwa kumuweka benchi kipa David De Gea, Real Madrid imezidi kutia
msisitizo kuwa inamtaka.
Kwa kuwa yuko benchi, basi anaonekana si chaguo la
kwanza na Madrid iko tayari kimwaga pauni milioni 25.
Wakati Man United inapambana na Tottenham katika mechi
yake ya kwanza ya Ligi Kuu England, De Gea alikuwa amekaa jukwaani pamoja na
makipa wengine wawili mkongwe Victor Valdes na Anders Lindegaard.
Hata hivyo tayari suala hilo limeishafikia ngazi za
juu za klabu hiyo baada ya Wakurugenzi wa Man United, Ed Woodward na yule wa Madrid,
Real Madrid Jose Angel Sanchez kukutana pamoja na wakala wa De Gea.
0 COMMENTS:
Post a Comment