August 8, 2015

Wakati Kocha Louis van Gaal ameamua kuanza Ligi Kuu England kwa kumuweka benchi kipa David De Gea, Real Madrid imezidi kutia msisitizo kuwa inamtaka.


Kwa kuwa yuko benchi, basi anaonekana si chaguo la kwanza na Madrid iko tayari kimwaga pauni milioni 25.
 
Wakati Man United inapambana na Tottenham katika mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu England, De Gea alikuwa amekaa jukwaani pamoja na makipa wengine wawili mkongwe Victor Valdes na Anders Lindegaard.

Hata hivyo tayari suala hilo limeishafikia ngazi za juu za klabu hiyo baada ya Wakurugenzi wa Man United, Ed Woodward na yule wa Madrid, Real Madrid Jose Angel Sanchez kukutana pamoja na wakala wa De Gea.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic