Kipa
mkongwe aliyeachwa Simba, Ivo Mapunda
amesema suala la kwamba hakutoa ushirikiano ni propaganda tu za viongozi.
Ivo
Mapunda amesema sababu ya Simba kutompa mkataba mpya kwa madai hakutoa
ushirikiano, hazina mashiko.
Kipa
huyo mkongwe, amechwa na Simba ambayo tayari ilishampa Sh milioni 8 kwa ajili
ya usajili.
“Kwa
kweli ni propaganda tu za viongozi. Mimi hilo haliniingii akilini kwamba
sikutoa ushirikiano.
“Nilikuwepo,
baadhi ya viongozi tulikuwa tukiwasiliana wakati nikipatiwa matibabu. Sasa sijui
hilo linatolea wapi,” alisema Mapunda ambaye kabla ya kutua Simba alikuwa Gor
Mahia.
Simba
imeamuacha Ivo na kuzua mjadala mkubwa lakini benchi la ufundi linaonekana
kuridhika na kipa mpya raia wa Ivory Coast.
0 COMMENTS:
Post a Comment