August 6, 2015

Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu ameanza kampeni ya waziwazi kwamba wachezaji wake watatu ndiyo wana nafasi ya kuwania tuzo ya mchezaji bora wa dunia.


Tuzo hiyo maarufu kama FIFA Ballon d'Or, sasa inashikiliwa na mshambuliaji nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo.

Josep amesema Lionel Messi anayepewa naafsi kubwa ya kuibeba, Luis Suarez na Neymar ndiyo wanaostahili.

Wachezaji hao wa Barcelona wote wanatokea katika bara la Amerika Kusini katika nchi za Argentina, Urugauay na Brazil.

Maneno ya Rais huyo wa Barcelona yanaonekana ni kama kampeni za mapema na makusudi.


Kama watatu hao wataingia fainali, halafu Messi akashinda, inakuwa ni sifa kubwa kwa Barcelona ambayo kibiashara ni msaada mkubwa kwa klabu hiyo kama ambavyo waliwahi kufanya Xavi, Iniesta na Messi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic