August 6, 2015

BOSSOU...
Beki wa kati wa timu ya taifa ya Togo, Vicent Bossou ametua nchini leo alfajiri tayari kujiunga na Yanga.




Bossou ni tegemeo katika kikosi cha Togo kinachoongozwa na nahodha Emmanuel Adebayor na kufundisha na kocha wa zamani wa Yanga, Tom Saintfiet.

Beki huyo wa kati ametua nchini siku moja baada ya Mzimbabwe, Thaban Kamusoko ambaye alikuwa akikipiga FC Platinum pamoja na mshambuliaji wa sasa wa Yanga, Donald Ngoma.

Timu ya mwisho ya Bossou inaonekana kuwa ni Goyang Hi FC ya nchini Korea na leo ametua nchini kufanya mazungumzo ya mwisho na Yanga.

Beki huyo ambaye pia aliwahi kukipiga Etoile du Sahel ya Tunisia anajiunga na Yanga kwa ajili aya kuimarisha safu ya ulinzi ambayo inaonekana kuyumba.



Yanga imemsajili Kamusoko kwa ajili ya kuyumba kwa safu yake ya kiungo cha ukabaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic