Baada ya Toto Africans ya jijini hapa kumpata
kocha mpya kutoka nchini Ujerumani, Martine Grelics, kocha huyo amefunguka na
kusema kuwa hatishwi na uwezo wa timu za Simba, Yanga na Azam FC na kudai kuwa
lengo yake ni kuhakikisha kuwa timu inafanya vizuri kwenye Ligi Kuu Bara.
Akizungumza ikiwa ni siku ya pili tangu kutua
nchini, Grelics alisema amekuja kufanya mabadiliko ndani ya kikosi cha Toto kwa
kuwafundisha falsafa mpya.
“Imani yangu ni kwamba endapo wachezaji
watanielewa basi Toto itakuwa tishio. Nimesikia uwepo wa timu kubwa hapa nchini
kama Yanga, Simba na Azam, hivyo nitakiandaa kikosi changu ili kiweze kuwa
mfano wa kuigwa kwa kuhakikisha kuwa timu inapata matokeo yatakayoifanya ipate
nafasi muhimu katika ligi,” alisema na kuongeza:
“Muda siyo mrefu tutaanza mazoezi magumu ambayo
yatasaidia wachezaji kwa jumla kuwa fiti na kuwa na nguvu.”
0 COMMENTS:
Post a Comment