August 7, 2015


Timu ya Simba imefanikisha usajili wa beki wa pembeni raia wa Burundi, Emiry Nibomana kwa dau la dola 10,000 (zaidi ya shilingi milioni 21).


Beki huyo mwenye uwezo wa kucheza namba 2 na 3, tayari alikuwa visiwani Zanzibar ambako timu yake hiyo iliweka kambi kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam, jana.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya uongozi wa timu hiyo, beki huyo anayetoka nchi moja na straika wa Yanga, Amiss Tambwe, amechukua kiasi hicho cha fedha akisaini mkataba wa miaka miwili ya kukipiga Msimbazi.

Chanzo hicho kilisema wakati Nibomana akichukua kiasi hicho kama dau la usajili, pia anatarajiwa kupokea dola 500 (sawa na shilingi milioni 1) kama mshahara wake wa mwezi.

Kiliongeza kuwa Nibomana aliyetokea Vital’O amesaini mkataba huo wa miaka miwili baada ya kufikia muafaka wa pande zote mbili kati ya mchezaji na viongozi kabla ya kusaini mkataba huo.

Alipozungumza na gazeti hili, mchezaji huyo alikiri kusaini mkataba na Simba kwa kusema: “Nimesaini mkataba wa miaka miwili na nipo tayari kwa ajili ya kupamba na ushindani utakaokuwepo kwa kuwa mimi mchezaji na hali kama hiyo ni ya kawaida.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic