Leo ndiyo Simba Day na Simba inacheza mechi ya
kirafiki dhidi ya SC Villa ya Uganda katika maadhimisho ya Tamasha la Simba Day
kwenye Uwanja wa Taifa Dar, straika wa timu hiyo Mussa Mgosi amesema
wamejipanga kutowaangusha mashabiki wao.
Mgosi amesema kwa kambi mbili walizopiga
Lushoto, Tanga na Zanzibar hivi karibuni kikosi chao kimebadilika na sasa kina
uwezo wa kuitetemesha timu yoyote.
Mgosi alisema atahakikisha anashirikiana vizuri
na wenzake ili Simba ishinde kufuta dhana ya kufanya vibaya katika mechi za
timu hiyo katika Simba Day.
“Binafsi naona maandalizi yameenda vizuri
kuanzia katika kambi ya Lushoto na hata Zanzibar kwa sababu tumecheza mechi za
kirafiki za kutosha, naamini kuwa zimetujenga vya kutosha,” alisema Mgosi.
“Nawaomba mashabiki waje kwa wingi kuiangalia
timu yao maana tunafahamu kuwa ni kipindi kirefu hawajaiona na haitakuwa vizuri
tukipoteza mbele yao, hivyo tutapambana ili tushinde.”
0 COMMENTS:
Post a Comment