Mshambuliaji wa Vital’O ya Burundi, Laudit
Mavugo, sasa amethibitisha kwa 100% kufa kwa dili lake na Simba baada ya
kurejesha fedha za awali alizopewa na Wekundu hao.
Mavugo ambaye awali alionyesha kutoafiki suala la
kurejesha fedha hizo akiamini lolote linaweza kutokea, amebadili mawazo na
kurudisha ‘advance’ ya dola 10,000 (Sh milioni 20) aliyotanguliziwa na Simba
kwa makubaliano ya kumaliziwa dola 10,000 nyingine baada ya kusaini.
Dili la Mavugo na Simba lilikufa baada ya Vital’O
kuongeza dau la usajili la mchezaji huyo kutoka Sh milioni 120 mpaka 200 baada
ya kuelezwa kuwa timu kibao zinamtolea udenda, hiyo ikaifanya Simba kukaa kando
na kuangalia mipango mingine.
Mtu wa ndani wa Simba amelivujishia Championi
Ijumaa ishu hiyo na jinsi walivyoahidiana na Mavugo kama itatokea wakati
mwingine wakihitaji huduma yake.
“Ameturejeshea ile pesa tuliyompa bila ya tatizo
na tumemalizana naye, tumeelewana kuwa kama baadaye tunaweza kuhitaji huduma
yake basi tutakamilisha hilo kwa wepesi zaidi maana hata hatukuelewa
kilichotokea kwa Vital’O kwenye dakika za mwisho,” alisema bosi huyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment