Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara (VPL) imetoka leo ambapo jumla ya timu 16 zinashiriki ligi hiyo
itakayoanza kutimua vumbi Septemba 12 katika viwanja tofauti nchini na
kumalizika Mei 7, 2016.
Kwa klabu ambayo haitawasilisha malipo ya ada ya mchezaji wa
kigeni ya dola elfu mbili (U$D 2000) mchezaji huyo hataruhusiwa kucheza kwenye
ligi hadi malipo hayo yatakapofanyika.
Michezo
saba itachezwa siku ya ufunguzi jumamosi katika viwanja tofauti ambapo Ndanda
Vs Mgambo Shooting (Nang’wanda - Mtwara), African Sports Vs Simba SC (Mkwakwani
- Tanga), Majimaji Vs JKT Ruvu (Majimaji - Songea), Azam FC Vs Tanzania (Azam
Complex - Dsm), Stand United Vs Mtibwa Sugar (Kambarage - Shinyanga), Toto
Africans Vs Mwadui (CCM Kirumba - Mwanza), na siku ya jumapili Young Africans
Vs Coastal Union (Taifa – Dar es salaam).
0 COMMENTS:
Post a Comment