Kipa Ivo Mapunda amesema
yuko tayari kusaini mkataba na Simba, lakini amekuwa haelewi kama kweli klabu
hiyo inamhitaji tena.
Akizungumza na
SALEHJEMBE, Ivo amesema kamwe hajakimbia kama ambavyo imekuwa ikielezwa.
“Nimekimbia vipi, mara ya
mwisho niliondoka kambini Lushoto baada ya kuumia. Collins (Kaimu Katibu Mkuu)
alinieleza atanipa mkataba.
“Nimekuwa nikisubiri na
hata niliwasiliana na kocha pamoja na Collins, bado inaonekana kuna
sintofahamu.
“Si kweli nimekimbia,
nipo tayari lakini vizuri nao wakaonyesha wana nia kweli ya kufanya kazi na
mimi,” alisema Ivo.
Kuhusiana na hilo, Rais
wa Simba, Evans Aveva amesema wanachosubiri na Ivo ni kusaini mkataba tu.
“Kuhusu Ivo
tulishamalizana, tunachosubiri kusaini naye mkataba. Hatukumpata kumalizana
naye lakini taarifa zinaeleza yuko jijini Dar.
“Hivyo itakuwa lahisi
kumpata na kumalizana naye. Baada ya
kusaini mkataba, basi tutawapa taarifa,” alisema Aveva.
Ivo aliumia wakati akiwa
Lushoto akalazimika kuondoka kambini kwenye kupata matibabu. Makubaliano yake
na Simba ni kuongeza mkataba wa mwaka mmoja, jambo ambalo linaelezwa
litafanyika kati ya leo, kesho na keshokutwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment