August 13, 2015


Kipa Ivo Mapunda amesema yuko tayari kusaini mkataba na Simba, lakini amekuwa haelewi kama kweli klabu hiyo inamhitaji tena.

Akizungumza na SALEHJEMBE, Ivo amesema kamwe hajakimbia kama ambavyo imekuwa ikielezwa.

“Nimekimbia vipi, mara ya mwisho niliondoka kambini Lushoto baada ya kuumia. Collins (Kaimu Katibu Mkuu) alinieleza atanipa mkataba.

“Nimekuwa nikisubiri na hata niliwasiliana na kocha pamoja na Collins, bado inaonekana kuna sintofahamu.

“Si kweli nimekimbia, nipo tayari lakini vizuri nao wakaonyesha wana nia kweli ya kufanya kazi na mimi,” alisema Ivo.
Kuhusiana na hilo, Rais wa Simba, Evans Aveva amesema wanachosubiri na Ivo ni kusaini mkataba tu.

“Kuhusu Ivo tulishamalizana, tunachosubiri kusaini naye mkataba. Hatukumpata kumalizana naye lakini taarifa zinaeleza yuko jijini Dar.

“Hivyo itakuwa lahisi kumpata na  kumalizana naye. Baada ya kusaini mkataba, basi tutawapa taarifa,” alisema Aveva.


Ivo aliumia wakati akiwa Lushoto akalazimika kuondoka kambini kwenye kupata matibabu. Makubaliano yake na Simba ni kuongeza mkataba wa mwaka mmoja, jambo ambalo linaelezwa litafanyika kati ya leo, kesho na keshokutwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic