Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi
ametuma salamu za pongezi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Burundi (FFB), Reverien Ndikuriyo kwa kuchaguliwa kuwa spika wa bunge la Seneta
nchini humo.
Katika salam hizo za pongezi kwa Rais wa FBF
na nakala zake kwenda Cecafa, Caf na Fifa, Malinzi ameelezea imani yake kwa
Seneta Ndikuriyo na amemtakia kila la kheri na mafanikio katika nafasi hiyo
mpya aliyochaguliwa.
Pamoja na kuwa ni nchi ndogo, Burundi imekuwa kati ya nchi zinazotoa vipaji vingi vya soka.
0 COMMENTS:
Post a Comment