RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI |
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limekiruhusu Chama cha Soka mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), kuendelea na mchakato wa
uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Soka Temeke (Tefa) kama
ulivyopangwa na kamati ya uchaguzi ya chama hicho.
Baada ya ruhusa hiyo Uongozi wa DRFA
umemuandikia barua Katibu Mkuu wa TEFA, Kassim Mustapha ili aijulishe kamati ya
uchaguzi ya chama hicho kuendelea na mchakato huo kama kawaida.
Awali, TFF iliiandikia barua DRFA kushauri
kusimamishwa kwa uchaguzi huo,kutokana na kile kinachoonekana kuwepo na
malalamiko kuhusu mchakato wake lakini maada ya mashauriano kati ya pande hizo
mbili,sasa ni ruksa kwa uchaguzi huo kufanyika kesho jumapili Agosti 16,2015
kama ulivyopangwa.
Aidha, DRFA imewaomba wapiga kura wote
kujitokeza kwenye uchaguzi,huku ikisisitiza amani na utulivu itawale katika
zoezi hilo muhimu la kuwapata viongozi watakaokiongoza chama cha soka
Temeke,ili kuleta maendeleo ya mpira wa miguu mkoa wa Dar es Salaam.
IMETOLEWA NA MSEMAJI WA DRFA, OMARY KATANGA
0 COMMENTS:
Post a Comment