August 5, 2015


Na Aidan Mlimila
Waingereza wana msemo wao mmoja wanasema "No longer at ease" ukiuleta katika lugha ya kiswahili una maana ya "Hakuna marefu yasiyo na ncha".Chochote kile ambacho kinakuwa na mwanzo lazima kitakuwa na mwisho pia.


Ni mda mrefu sasa tangu Jose Mourinho alipoanza kumnyanyasa kocha wa Arsenal,Arsene Wenger.

Tangu mwaka 2004 Jose Mourinho alipojiunga na Chelsea akitokea Fc Porto ya Ureno, Wenger alikuwa hajawai kumfunga Mourinho katika mechi 13 walizokutana mpaka mwisho wa msimu uliopita Wenger alikuwa hajawai kushinda zaidi ya kuambulia sare.

Hii ina maana Arsene Wenger alikuwa hajawai kupata matokeo chanya dhidi ya Mourinho kwa takribani dakika 1,170. 

Mourinho amekuwa akimnyanyasa Wenger ndani na nje ya uwanja ukiachilia mbali uwezo wa kimbinu aliokuwa nao Jose ndani ya uwanja lakini pia ana kipaji kikubwa mno cha kuzungumza na kucheza mind games kitu ambacho kwa kiasi kikubwa amekuwa akimshinda Arsene Wenger.

Siku ya jumapili iliyopita tar 2 ilikuwa ni siku ambayo Wenger alikuwa anatoka kwenye kifungo ambacho alikuwa kwa mda mrefu na ilikuwa ni baada ya kufanikiwa kumfunga mtu ambaye amekuwa akimnyima raha na kubeba taji la ngao ya jamii(Community Shield). Atleast kwa sasa Wenger anaweza kupumua kutoka kwenye manyanyaso ya Mreno Mourinho.

Nikiitazama Arsenal kwa misimu miwili hii inaonekana kuwa na mabadiliko pale wanakuwa wanacheza mechi kubwa(Big matches) kwa misimu michache ya nyuma Arsenal wamekuwa wakipata tabu sana kupata matokeo katika mechi kubwa hata kwa zile mechi ambazo wao wanakuwa wamepewa nafasi kubwa ya kushinda.

Uhasama wa Jose na Wenger ulioonekana kuongezeka sana pale Jose alipomwita Wenger mtalaamu/bingwa wa kufeli(specialist in failure) kitu kilichopelekea wawili hawa kushikana mashati wakati timu hizi zikipokutana pale darajani.

Wachezaji wengi wa Arsenal kwa sasa wanaonekana kukomaa na hata ule uwoga ambao wamekuwa nao hasa pale wanapocheza mechi kubwa kwa sasa unaonekana kuisha kitu kinachonifanya nianze kuamini na kuona kama ule uteja ambao Wenger alikuwa nao kwa Mourinho unaanza kutoweka kama siyo umeshatoweka.


Ingawa bado nadhani Arsenal inabidi wafanye kazi kubwa sana ili waweze kushinda taji la ligi kuu kitu ambacho kimekuwa kikiwasumbua kwa mda mrefu sasa tangu watwae taji la mwisho msimu wa 2003/04.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic