KIKOSI CHA NDANDA MSIMU ULIOPITA... |
Wakati dirisha la usajili likitarajiwa kufungwa
wiki ijayo, Ndanda FC ya Mtwara ipo katika mazungumzo na kiungo mshambuliaji,
Oziri Desmond, raia wa Nigeria, aliyeletwa nchini na mmoja wa viongozi wa Yanga
SC.
Mchezaji huyo mwenye mwili uliojengeka kimazoezi,
anafanya majaribio na Ndanda FC chini ya Kocha Ngawina Ngawina na kama
ataliridhisha benchi la ufundi la timu hiyo, atafanikiwa kusaini mkataba.
Desmond ameliambia gazeti hii kuwa, mchezaji huyo
ameunganishwa kuja nchini kwa msaada wa Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, baada ya
kukutana naye katika mitandao ya kijamii.
“Ninapenda mazingira ya Tanzania, ingawa nina
muda mfupi tangu nifike hapa. Awali sikuwa nikifahamu chochote kuhusu hapa,
lakini ninamshukuru Hafidh Saleh wa Yanga ndiye aliyenisaidia.
“Aliniambia atanipeleka Mbeya City lakini
ilishindikana, ingawa sifahamu nini kilikwamisha, ndipo akaamua kunileta huku
(Ndanda) ambapo napo wamenipokea vizuri, nina uhakika nitapata nafasi.
“Saleh nilikutana naye katika mitandao,
akaniambia nimtumie video zangu, nikafanya hivyo ndiyo akanifanyia mpango,”
alisema Mnigeria huyo.
Kabla ya kutua Ndanda, Mnigeria huyo amesema
alicheza katika timu za Doan FC na Mayzz FC, zote za Yemen, pamoja na Mighty
Blackpad ya Sierra Leone.
0 COMMENTS:
Post a Comment