August 8, 2015


Kocha wa Yanga Mholanzi, Hans Pluijm ameonekana kuanza kuisuka upya safu yake ya ushambuliaji ya timu hiyo huku akigawa majukumu kwa mawinga na mabeki wake wa pembeni.

Hiyo ni siku chache tangu timu hiyo iondolewe kwenye michuano ya Kagame katika hatua ya robo fainali dhidi ya Azam FC kwa kufungwa kwa penalti 5-3.

Safu hiyo ya ushambuliaji inaongozwa na Mzimbabwe, Donald Ngoma, Amissi Tambwe (Burundi) na Malimi Busungu huku mawinga wakiwa ni Simon Msuva, Deus Kaseke, Andrey Coutinho (Brazil) na Geoffrey Mwashiuya na mabeki ni Hajji Mwinyi na Oscar Joshua.

Kocha huyo, alionekana akiisuka upya kombinesheni hiyo kwenye mazoezi ya jana Ijumaa, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam akisaidiana na Charles Mkwasa.

Katika mazoezi hayo, Pluijm aliwagawa washambuliaji hao wawiliwawili na kukimbia golini kwa kupishana kuwahi na kuiunganisha mipira ya krosi iliyokuwa inapigwa na mawinga.

Ngoma na Tambwe walipangwa pamoja ambao walikuwa wakikimbia kwa kupishana kuwahi mipira hiyo ya krosi ndani na nje ya 18 kwa ajili ya kuwahi mipira hiyo ya krosi kwa ajili ya kufunga.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, Pluijm alisema kuwa “Katika Kombe la Kagame nimeona kuna vitu havipo sawa katika safu ya ushambuliaji, ndiyo kama ulivyoona najaribu kuweka mambo sawa.”

“Nimepanga kuboresha kikosi changu kwa kila sehemu kwa kuanzia safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji, ninataka timu ifanye mashambulizi ya kushtukiza kwenye goli la timu pinzani huku tukilinda goli letu.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic