Hatimaye, Tottenham imeachana rasmi na mshambuliaji raia wa
Togo, Emmanuel Adebayor.
Taarifa kutoka katika klabu hiyo zimeeleza, Adebayor na
Spurs wameachana baada ya kufikia makubaliano.
Lakini Adebayor atalazimika kukaa bila ya kuichezea timu
yoyote hadi Januari, mwakani litakapofunguliwa dirisha la usajili.
Awali, Adebayor aligoma kuondoka Spurs hadi atakapolipwa
pauni milioni 5 kama inavyoeleza katika mkataba wake.
Hata hivyo klabu hiyo iliona fedha hizo ni nyingi sana. Inaelezwa
hata katika makubaliano hayo, Adebayor alikubali kutoa punguzo la dola milioni
2.
Ingawa klabu wala Adebayor mwenyewe, hakuna aliyekuwa tayari
kweka wazi kuhusiana na hilo.
West Ham United ndiyo inayoonekana kumtaka na kuna uwezekano
mkubwa wa kujiunga nayo Januari, mwakani.








0 COMMENTS:
Post a Comment