September 22, 2015

PICHA YA SIMU ILIYOPIGWA YANGA WAKIFANYA MAZOEZI MJINI PEMBA

Yanga wako mjini Pemba, tayari wameanza mazoezi kujiwinda na mechi yao ya Jumamos dhidi ya watani wao Simba ambao wako mjini Zanzibar.


Kikosi cha Yanga, tayari kimeanza mazoezi kwenye Uwanja wa Gombani, lakini ajabu, hawataki kupigwa picha.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amewaambia waandishi kwamba haitakiwi kupiga picha mazoezi.

“Haya ni maelekezo ya uongozi, hivyo hatutazungumza wala hatutaki picha,” alisema Hafidhi.

Hata hivyo, waandishi walipinga hilo na kuwataka Yanga kuwapa nafasi ya kufanya kazi yao.


Jambo hilo lilizua mzozo kati ya kiongozi huyo na waandishi huku mashabiki wakitaka waandishi wapewe nafasi ili Wanayanga wajue timu yao inaendeleaje kwa kuwa sasa iko mbali na sehemu kubwa ya Tanzania wanataka kujua inaendeleaje.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic