September 22, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluim amewataka wachezaji kusahau kabisa kuhusiana na suala la mabao 5-0 waliyofungwa na Simba.


Akizungumza kutoka mjini Chake Chake, Pluijm ameitaka Yanga kusahau kipigo hicho cha Simba ili wagange yajayo.

“Kufungwa katika soka ni jambo la kawaida kabisa. Huu ndiyo wakati wachezaji wanapaswa kusahau yale masuala ya kipigo hicho.

“Ukitaka kuwafunga Simba, kwanza lazima usahau kipigo cha mabao matano. La sivyo tutaendelea kubaki hapa,” alisema.

Pluijm na Yanga wako mjini Chake Chake kisiwani Pemba kujiandaa na mechi dhidi ya watani wake Simba.

Mechi hiyo ya watani itakayopigwa Jumamosi, inasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wengi tena kwa hamu kubwa.
Simba imejichimbia mjini Unguja kwa ajili ya mechi hiyo pia ambayo kila timu inataka kuendeleza ushindi baada ya kuanza na ushindi katika mechi zote tatu za mwanzo.
Tayari Yanga wameanza kujifua kwenye Uwanja wa Gombani 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic