Uongozi wa
Azam FC umeonyesha kuwa una thamini kwa kiasi kikubwa uhuru wa wachezaji wake.
Hali hiyo
inatokana na uamuzi wa kutaka kuona wachezaji wake wanapiga kura katika
uchaguzi Mkuu wa Jumapili Oktoba 25 kwa kuamua kuwasafirisha usiku.
Azam FC
inashuka dimbani Alhamisi kuivaa Ndanda FC kwenye Uwanja wa Nangwanda kuwavaa
wenyeji Ndanda FC.
Baada ya
hapo, itaanza safari ili wachezaji wake wawe jijini Dar es Salaam mapema
kujiandaa na suala la upigaji kura Jumapili.
“Lengo
letu ni kuhakikisha wachezaji wetu wanapata nafasi ya kupiga kura kwa uhakika
kwa kuwa ni haki yao,” alisema Saad Kawemba, mmoja wa wakurugenzi wa Azam FC.
0 COMMENTS:
Post a Comment