Kiungo Yaya Toure ambaye ni mchezaji bora
Afrika, ameendelea kusisitiza kuwa hana raha katika kikosi cha Manchester
United.
Toure aliwahi kuzozana na Man City kabla ya
kukubaliana na City na baadaye kuendelea kubaki.
Toure ,32, amekuwa akiwaeleza rafiki zake kwamba
hayuko katika hali inayompa furaha hata kidogo.
Amekuwa akionekana kutokuwa na furaha ingawa
ukimya wake unamfanya aonekane kama yuko katika mazingira ya kawaida.
Katika mahojiano na gazeti namba moja la michezo
duniani la L’Equipe, Toure amesema hana raha tokea amefika Man City.
“Nilipokwenda City, watu waliona nimekosea,
wakanicheka lakini baadaye tukachukua makombe na kuwa gumzo.
“Ajabu hadi sasa hakuna watu hawaoni
tulichofanya na hawaonyeshi kukubali,” alisema.
Hata hivyo Toure hakuweka kila kinachomfanya
asiwe na furaha.
0 COMMENTS:
Post a Comment