October 15, 2015


Bondia Francis Cheka amevuliwa ubingwa wa dunia alioutwa baada ya kumtwanga bondia kinyozi kutoka nchini Marekani.
Cheka amevuliwa ubingwa huo kwa sababu mbili zilizoelezwa kujitokeza.
Jay Msangi aliyeandaa pambano hilo, alisema Cheka alivuliwa ubingwa baada ya kwenda kucheza pambano nchini Russia ambalo halikuwa la ubingwa.
Lakini Cheka ameiambia SALEHJEMBE kwamba kitendo cha kukaa bila ya kupigana ndicho kilichochangia kuvuliwa.

“Hilo la Russia linaweza kuchangia, lakini ukweli muda wa kuutetea ubingwa ulipita, hakukuwa na promota wa kuniandalia pambano.

“Ndiyo maana nikavuliwa ubingwa na hadi unapoona hapa, si bingwa tena wa dunia wa WBF, inajiuma sana,” alisema Cheka ambaye ni bondia bora zaidi nchini kwa kipindi hiki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic