KIBADENI |
Baada ya kikosi cha JKT Ruvu kumkabidhi timu
kocha na mchezaji wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni ‘King’, imebainika
ataifundisha timu hiyo bila kuwa na mkataba kutokana na kukabiliwa na majukumu
mengine.
Mara baada ya kukabidhiwa majukumu hayo, Kibadeni
akaomba kocha msaidizi wa zamani wa Kagera Sugar, Mrage Kabange awe msaidizi
wake, jambo ambalo halikupingwa, lakini kutokana na majukumu mengine yakiwemo
ya kituo chake cha soka cha KISA (Kibadeni Soka Academy) kilichopo Chanika
jijini Dar es Salaam, akaomba kutopewa mkataba ili kutojibana.
“Nimekubali kuisaidia timu, masuala ya fedha
nimeweka kando ingawa sitakuwa na timu muda wote kutokana na kuwa na majukumu
mengine. Ndiyo maana nilipoombwa kufanya kazi nikaomba niwe na Kabange kwa kuwa
namjua vizuri utendaji wake,” alisema Kibadeni na kuongeza:
“Kuna muda (JKT Ruvu) watakuwa wanakuja kwenye
academy yangu kufanya mazoezi, maana kuna wachezaji wenye vipaji na sitaki
vipotee.”
0 COMMENTS:
Post a Comment