Kocha
Luis Enrique wa Barcelona amesema wanafanya kazi ya ziada kuboresha safu yao ya
ulinzi.
Enrique
amesema benchi la ufundi wanafanya kazi hiyo na itakuwa inaboreshwa kila
wanavyoendelea kucheza.
“Kuna
mechi kadhaa tulionyesha kuwa tuna matatizo katika safu ya ulinzi. Sasa
tunataka kulimaliza kabisa hilo tatizo,” alisema Enrique.
“Lakini
lazima tuendelee kujifunza na kubadilisha, hatuwezi kubadili kila kitu kwa siku
mbili,” alisema.
Barcelona
imekuwa ni moja ya timu zilizoruhusu mabao mengi katika mechi zake 10
zilizopita.
Wengi
wamekuwa wakimtuhumu beki Gerard Piqeu kushuka kiwango.
0 COMMENTS:
Post a Comment