Na Paul Mwakipesile, Mbeya
Pamoja
na Simba kuonyesha wanajiamini kabla ya kuivaa Prisons, kesho lakini wazi hofu
imetanda.
Kocha
Simba, Dylan Kerr ametamba kwamba watawafunga Prisons licha ya kwamba haijui
timu hiyo.
Lakini
jana mjini hapa kulikuwa na ulinzi mkali katika mazoezi ya Simba na waandishi
walikataliwa kuingia.
Pamoja
na kufanya kwenye Uwanja wa JKT mjini hapa, viongozi wake wa hapa walizuia
waandishi kuingia.
Juhudi
za waandishi angalau kutaka kupiga picha tu ziligonga mwamba, ikionyesha wazi
Simba walikuwa na hofu kuhusiana na Prisons.
Prisons itashuka kwenye Uwanja wa Sokoine kesho ikiwa na hasira ya kupokea kipigo cha mabao 3-0 ugenini mjini Shinyanga dhidi ya Stand United katika mechi yake ya mwisho ya Ligi Kuu Bara.
0 COMMENTS:
Post a Comment