Kocha Mkuu wa
Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa amesema angalau akipata siku 10 za
maandalizi kwa ajili ya kikosi chake anaweza kufanya vema dhidi ya Algeria.
Stars itaivaa
Algeria Novemba, mwaka huu katika mechi ya kuwania kucheza Kombe la Dunia.
Stars imepata
nafasi hiyo baada ya kuitoa Malawi kwa jumla ya mabao 2-1 katika mechi mbili za
jijini Dar es Salaam na baadaye Blantyre.
Mkwasa
ameiambia SLAEHJEMBE kwamba anajaribu kufanya jitihada angalau siku 10
zipatikane kwa ajili ya maandalizi.
“Siku kumi
angalau zinaweza kutupa picha. Kwa kawaida hadi sasa kuna simu tatu za
maandalizi ambazo naamini hazitoshi.
“Kama simu hizo
kumi zitapatikana, nitafurahi sana kwa kuwa itakuwa ni msaada kwa maana ya
maandalizi,” alisema Mkwasa.
Kabla ya kuivaa
Nigeria kuwania kucheza Afcon na baadaye Malawi kuwania kucheza Kombe la Dunia.
Stars iliweka kambi kwenye mji wa Kartepe nchini Uturuki na matunda
yakaonekana.
0 COMMENTS:
Post a Comment