Kocha
Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema kazi bado ni ngumu pamoja na
mwenendo mzuri wa kikosi chake.
“Ligi
haiwezi kupungua ugumu, itakwenda hivi. Hata kama kuna timu zitajigawa kwa
maana ya ubora lakini haziwezi kuwa
chache.
“Hata
ukiwa na timu tano au sita katika ligi ambazo ni imara, maana yake ligi ni
ngumu na inatakiwa kupambana mwanzo ahdi mwisho,” alisema Pluijm.
Yanga
imecheza mechi sita, imetoka sare moja na sasa iko kileleni ikiwa na pointi 16,
sawa na Azam FC.
Yanga
na Azam FC ndiyo timu pekee ambazo hazijapoteza hata mechi moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment