Watu wanazeeka
na mambo yao, Paul Scholes akiwa na umri wa miaka 40, amefanya yale aliyokuwa
akifanya wakati kinda.
Scholes amepiga
shuti kali umbali wa mita 35 huko Hong Kong na kufunga bao safi kabisaa.
Ilikuwa ni
mechi ya hisani kati ya wachezaji wa zamani wa Ligi Kuu England dhidi ya
kombaini ya wenyeji.
Scholes akiunga
kikosi hicho na wachezaji wengine baadhi kama Emmanuel Petit, Claude Makelele,
Robert Pires, Darren Anderton na Robbie Fowler.
Wakati
akiichezea Man United, Scholes alikuwa maarufu kwa pasi ndefu zenye uhakika,
pia mashuti makali.
DAILY MAIL
DAILY MAIL
0 COMMENTS:
Post a Comment